Tutumie message yenye neno"KAMPUNI" Whatsapp namba +255764530882 kupata maelezo zaidi juu ya huduma yetu* Karibu Sana TJ CONSULT & CO.LTD kwa kazi zote za Graphics design ... Tuna design Logo, Company profile



Habari Mjasiliamali na mpambanaji, Inawezekana bado unajiuliza na kujishauri kuhusu umiliki wa kampuni au urasimishaji wa biashara zako lakini bado hujafikia muafaka, na pengine hujawahi hata kufikiria kabisa na hapa huenda ikawa ni mara yako ya kwanza kufahamu kuhusu makampuni, hali hiyo hupelekewa na sababu mbalimbali ikiwemo kutokujua kabisa, yaani mtu mwingine akisikia neno ‘Kampuni’ tayari yanamuijia kichwani kwake majengo makubwa, magari, wafanyakazi wengi watanashati, akaunti ya fedha benki yenye pesa nyingi, n.k. hivyo mtu huyo hujiona yeye sio hata wa kulitaja neno kampuni.
Pia sababu nyingine kutokuelewa ni namna gani biashara zake zinaweza kusajiliwa na kuendeshwa kama kampuni, na zaidi ni kutokuelewa umuhimu wa kuwa na kampuni, yaani unakuta mtu anafanya biashara nyingi na kubwa mfano kusafirisha mbao kutoka mkoa wa Iringa kuleta Jijini Dar es Salaam, au kutoa samaki Mwanza kuleta Dar es Salaam, au biashara ya kukopesha pesa, n.k. lakini anaona biashara zinakwenda vizuri tu na hivyo asione hata umuhimu wa kuzirasimisha biashara zake.

Unapoamua kufanya biashara ni vema kuzingatia mfumo wa usajili wa biashara yako na kuamua vema ili kufanya biashara katika mazingira mazuri hususani ya kisheria, ndiyo sababu TJ CONSULT & CO.LTD huwa tunawashauri kwa weledi wale wanaosajili biashara zao ili wafanye maamuzi sahihi. Kwa kifupi, unaweza kusajili Jina la biashara, mfano ‘Ifakara intersperses’, endapo nikiwa nafanya biashara ya kusafirisha mizigo, au ‘Ifakara Microcredit’ endapo ninafanya biashara ya kukopesha pesa, na nitaruhusiwa kuendesha shughuli za biashara (Business activities) kuanzia moja mpaka Nne tu, endapo nimesajili Jina la biashara.biashara

*Lakini leo nitajikita katika Kampuni, na mada ya Kampuni ni kubwa mno, ila nitakufafanulia faida chache muhimu za kuisajili biashara yako kama kampuni, kwani wengi huuliza, “kuna faida gani za kuwa na kampuni?”*
kama nilivyotangulia kusema hapo juu kuwa jina la biashara linakupa ruhusa ya kufanya shughuli za biashara zisizozidi nne, tofauti na kampuni ambapo unaweza kuorodhesha shughuli za biashara mpaka 50, yaani hata zile ambazo unatarajia kuzifanya kipindi kijacho, zinaweza kutambulika sasa na hapo baadae likabaki suala la upatikanaji wa leseni ya biashara hiyo kwenye halmashauri za manispaa au wizarani pamoja na vibali husika kutoka kwenye mamlaka za serikali, mfano TFDA, TBS na kadhalika.


Moja kwa moja tuangalie umuhimu wa kusajili kampuni, Mara kwa mara huwa napokea simu za wateja wetu wengi sana wengine wannitumia ujumbe, wengine hunicheki whatsapp, wengine kwenye E-mail yangu, maswali wanayoniuliza ni kuhusu faida za kufungua kampuni, huwa nawaeleza kwa ufupi lakini huwa wanaonekana kutaka kufahamu zaidi suala zima la kodi, kwasababu suala hili la kodi limekuwa likiulizwa na wengi sana, pia wafanya biashara wengi wamekuwa wakihitaji kufahamu kuhusu kodi za makampuni, wajasiriamali na wafanya biashara na wengine wengi nimekuwa na majadiliano nao kuhusu suala hili, nitajitahidi kueleza kwa undani na kwa ufupi kama ifuatavyo:
Kodi ya makampuni ni kodi inayotozwa katika mapato yanayotozwa kodi (faida) ya asasi kama vile makampuni yenye dhima ya ukomo. Kampuni yenye dhima ya ukomo (Limited Liability company) inalipa kodi ya shirika (Corporate Tax) ambayo ni 30% kwa viwango vya sasa kutokana na Sheria ya mapato iliyofanyiwa mapitio mwaka 2008 na kodi hii hukokotolewa kwenye faida ya mwaka, hivyo basi, kampuni itakuwa na unafuu mkubwa kwenye kiwango hiki ukilinganisha na endapo biashara hiyo ingekuwa ina umiliki binafsi(Jina la biashara), hasa hasa pale ambapo kampuni inazidi kukua na kuongeza shughuli za biashara.

Kwa mujibu wa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), mapato yanayotozwa kodi (faida) katika kodi ya makampuni yanahusisha: 
1. Faida inayotokana na shughuli za biashara, 
2. Faida inayotokana na uwekezaji (isipokuwa migawanyo ya faida ambayo imetozwa kodi tofauti kama kodi ya mwisho),
3. Kodi inayotokana na mapato ya makampuni yenye hasara za muda mrefu ambazo hazijasamehewa kwa miaka mitatu mfululizo. 

Mpenzi msomaji wa makala hii, fahamu kwamba zipo faida nyingi zitokanazo na uendeshaji biashara kama kampuni, kwani makampuni hunufaika na misamaha ya kodi pamoja na mapunguzo ya kodi kutokana na aina ya shughuli mbalimbali ambazo inajihusisha nazo.
Kwa mfano, kwa mujibu wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), Kampuni mpya iliyoanzishwa na ambayo inajihusisha na utengenezaji wa madawa ya binadamu na bidhaa za ngozi na ina mkataba wa makubaliano na Serikali ya Jamhuli ya Muungano wa Tanzania itatozwa kodi kwa kiwango cha 20% kwa kipindi cha miaka mitano mfulizo kutoka mwaka walipoanza uzalishaji, hii ni pungufu ya 10%, pia kama kampuni haijapata faida, itaandaa vitabu vyake vya mahesabu na kuviwasilisha kwenye mamlaka ya mapato na haitalipa chochote, kodi itatozwa kwenye faida kama ilivyoainishwa kwenye sheria na si vinginevyo, tofauti na biashara binafsi(sole proprietors).

Watu binafsi (sole proprietors) hukadiriwa kodi kutokana na mauzo yao, kwa mfano; 
Kwa mtanzania (bara) kodi kwa mtu binafsi endapo mapato yake yanazidi Shs 720,000/= kiwango cha kodi anayotozwa ni Shs 98,100/= jumlisha na 30% ya mapato yanayozidi Shs 720,000/=, lakini kwa kampuni, huenda mapato yakawa ni hiyo hiyo Shs 720,000/= kwa mwezi, na gharama na matumizi vikawa ni Shs 300,000/=, kwa hiyo faida ni Shs 420,000/=, kwa hiyo kwa mwezi huo kwa kampuni kodi itakokotolewa kwa kupata 30% ya faida, yaani Shs 420,000/= ambayo ni Shs 126,000/=, tofauti na mtu binafsi ambaye atalipa Shs 98,100/= jumlisha 30% ya mapato yanayozidi 720,000/=, tuseme ni Shs 800,000/= ambayo ni Shs 240,000/=, hivyo kutakiwa kulipa kiasi cha Shs 338,100/=. japo kwa mwaka mapato yasiyozidi Shs 2,040,000/= kwa watu binafsi hayatozwi kodi, lakini kwa hali ya kawaida ya biashara na bei ya vitu na huduma kuwa juu, ni rahisi kwa mapato kuzidi kiwango hicho pamoja na kupata faida kidogo, lakini kwa kuwa ni mtu binafsi mzigo wa kodi ukakuelemea vile vile.
Kwa hiyo, hapa tunaona unafuu wa kusajili kampuni, na ndivyo ambavyo Shinebright Consulting tunawashauri wawekezaji, na ukihitaji kufahamu zaidi wasiliana nasi au tutembelee ofisini.

Pia, Unapoisajili biashara yako kuwa kampuni unapunguza hatari ya kuwepo kwa mvutano wa kimaslahi baina ya waanzilishi, kwani wamiliki wa kampuni maslahi yao kwenye kampuni husika ambayo wanaimiliki yanakoma kulingana na idadi ya hisa wanazozimiliki, au kiwango cha uwekezaji kutokana na hisa walizozinunua, na si vinginevyo. Tumezoea kuwepo na makubaliano holela ya mdomo au maandishi kwamba mtu A na mtu B wamekubaliana watafanya biashara fulani kisha watagawana faida, halafu baadae wanaanza kuingia kwenye migogoro kwamba huyu anasema biashara ni ya kwake na yule anasema ni ya kwake, au katika kugawana faida kila mmoja anaweza kumzidi mwenzake na hupelekea watu kugombana hata kusababisha hasara kubwa, lakini kama watu wameamua kufanya biashara kwa kuisajili kwanza kuwa kampuni, biashara hiyo inakuwa na utaratibu rasmi wa kisheria katika kuisimamia na anapotaka kujiondoa mmoja wapo, unafuatwa utaratibu rasmi ambao upo kwa mujibu wa sheria, na si vinginevyo.
Hivyo basi, kusajili kampuni kunaondoa migogoro mingi ambayo inaweza kujitokeza baadae, hasa biashara inapokua kubwa sana au inapoonekana kukwama kukua.

Hali kadhalika kusajili kampuni kunapelekea kuwepo na mazingira rafiki ya kukuza mtaji. Kuongeza mtaji wa kampuni kunaweza kusaidia katika upanuzi wa biashara au kupelekea ukuaji. Taratibu za kitaalamu na kisheria zimeainisha namna nzuri za kuongeza mtaji aidha kwa kuuza hisa zilizobakia kwenye kampuni kwa wamiliki waliopo ili kuongeza mtaji, au kwa kuongeza wanahisa wapya na kununua hisa za kampuni ili kuongeza mtaji, na pia ni rahisi hata kuwakaribisha wawekezaji wengine ndani au nje ya nchi wakanunua hisa na kuongeza mtaji bila kuathiri shughuli za kampuni. 
Sio rahisi kama mtu unafanya biashara ambayo haijasajiliwa kuwa kampuni, kuwakaribisha watu wengine kuwekeza pesa zao kwako, usalama wa kuwekeza pesa ni pale ambapo biashara imesajiliwa kama kampuni, kwani hata katika macho ya kisheria kampuni inatazamwa kama taasisi nyingine tofauti na wamiliki wa kampuni hiyo (separate entity).

Jambo lingine muhimu kabisa ni kuwepo kwa ukomo wa dhima binafsi (Limited liability). 
Kampuni mbele ya macho ya sheria ni taasisi inayosimama yenyewe tofauti na wamiliki wa kampuni hiyo (separate legal entity), na kampuni inaweza kushitaki au kushitakiwa mahakamani (veil of incorporation), hivyo basi, endapo biashara inapata misukosuko katika uendeshaji, umiliki au uwekezaji, n.k. inaweza kuwajibika yenyewe na wamiliki wa kampuni hiyo wasipoteze kitu chochote isipokuwa tu uwekezaji wao kwenye kampuni hiyo. Mfano; katika biashara, mmekopa pesa benki au kwenye taasisi yoyote ya fedha na biashara ikashindwa kufikia malengo ikajikuta inaingia kwenye madeni makubwa, ni kampuni ndiyo itakayowajibika kwenye madeni hayo, na wamiliki wa kampuni watakachopoteza ni uwekezaji wao kwenye kampuni husika. Pia endapo bidhaa au huduma zilizotolewa zimeisababishia hasara kampuni, itakayowajibika ni kampuni yenyewe. Hii ni tofauti na biashara binafsi (Sole proprietorship) ambapo mmiliki wa biashara anawajibika moja kwa moja yeye mwenyewe kwasababu kisheria ni yeye mwenyewe ndiye anayetambuliwa na si vinginevyo.

Mwisho tuangazie suala muhimu sana nalo ni kujitambulisha na kujitengenezea hadhi kibiashara, jambo ambalo linaweza kuboresha mahusiano mazuri baina ya kampuni yako na wateja (Branding). Leo tunaona makampuni makubwa kama Vodacom, IPP Media, Mbeya Cement, CRDB n.k. namna yalivyojitengenezea namna ya kutambulika kwa wateja wao, unapolisikia tu jina la kampuni mojawapo limetajwa unapata picha halisi na kubwa juu ya biashara ya kampuni hiyo kwa uharaka. Kuendesha biashara iliyosajiliwa kama kampuni pia kunakupelekea kuaminika na ni rahisi hata kuingia mikataba mikubwa aidha na makampuni mengine au na serikali. Kwa mfano, serikali inatangaza zabuni ya ujenzi wa barabara na mradi huo gharama yake ni Shs 30,000,000/=, pesa hizo zote sio rahisi kuingia mkataba na mtu binafsi au watu wachache binafsi wasio rasmi kisheria, lakini ni rahisi kuingia mkataba na kampuni, na pia hata kukopeshwa kwenye mabenki na makampuni ya fedha mikopo mikubwa ya biashara ni rahisi endapo mmesajiliwa kama kampuni kuliko binafsi (individuals).

Leo TJ CONSULT & CO.LTD imekuwa na nafasi kubwa ya kuhudhuria mikutano mikubwa na kukutana na wawekezaji wa nje wengi na wa ndani wengi ambao wanamtazamo mpana kibiashara na tumekuwa tukiwashauri wawekezaji wa ndani na nje ya nchi namna ambavyo wanaweza kunufaika endapo watasajili biashara zao kuwa kampuni na sio kuziendesha kiholela au kienyeji.
Jambo moja ambalo nilitaka kulisahau, unaposajili kampuni inakurahisishia wewe hata namna ya kuirithisha biashara, kwa mfano; Baba na mama mmesajili kampuni na mtoto wenu amefikisha umri wa miaka 18, mnaweza kumuongeza kama mwenye hisa (Shareholder) na biashara zikaendelea kama kawaida, wakati anaendelea kupata elimu, anakuwa anafahamu fika kwamba anasoma ili asimamie biashara ambayo yeye mwenyewe ni mmiliki halali wa sehemu ya biashara hiyo kutokana na kiwango cha hisa anazozimiliki, hivyo kumfanya asome kwa bidii bila kuwa na hofu juu ya soko gumu la ajira.
Zipo faida nyingi na muhimu sana za kusajili biashara yako kuwa kampuni, usichelewe kwani wakati ni sasa, rafiki yangu mmoja nilimsikia akisema kuwa “Kusajili kampuni ni lazima uwe na gari kwanza, lazima” aliongea kwa kusisitiza, lakini kwa kumsaidia na kwa faida ya wengi, kusajili kampuni zipo taratibu maalum zilizowekwa na mamlaka husika yaani BRELA (Wakala wa usajili wa makampuni na majina ya biashara), na sisi kama washauri nafasi yetu ni kukushauri uwe na ufahamu juu ya makampuni na uendeshaji wake, umuhimu wa kusajili biashara na kukupa msaada wa kitaalam ili uweze kufanya maamuzi sahihi na yenye tija, ili kutimiza malengo yako kwa wakati na bila gharama zinazoepukika.
Mimi ni Business doctor, Life coach na mchambuzi wa masuala ya biashara na mjasiriamali.
*TJ CONSULT & CO.LTD*
*Kama una wazo la kufanya biashara hapa Tanzania na ungependa kumiliki kampuni yako au jina la biashara lako,* huduma yetu ni kukusaidia kufanikisha usajiri wa biashara yako. Tutumie message yenye neno "KAMPUNI"  Whatsapp namnba +255764530882  kupata maelezo zaidi juu ya huduma yetu*
Karibu Sana TJ CONSULT & CO.LTD kwa kazi zote za Graphics design ... Tuna design Logo, Company profile, kwa wajasiliamali, Matangazo ya mtandaoni, Business card, rollup banner,catalog, hotel & restaurant menu, business proposal, company profile na vingine vingi, Huduma zetu sisi TUNAKUFIKISHIA POPOTE ULIPO.
Call 255626 402 722 OR +255764530882, WhatsApp no: +255764530882,
TJ Tuna aminika kufanya Graphics Design kwa Kwa bei zakawaida kabisa kwa asilimia 100% karibuni sana TJ CONSULT & CO.LTD

*SASA NAHITAJI KUTENGENEZA COMPANY PROFILE NA KUSAJIRI KAMPANI YANGU,NITAWAPATA WAPI TJ CONSULT & CO.LTD*??
*Tumia hayo mawasiliano hapo chini kuwasiliana na TJ CONSULT & CO.LTD au fika offisini kwetu Tunapatikana, SONGEA MFARANYAKI & DODOMA NKUHUNGU;*

Whatsapp & call +255764530882,+255626 402 722

E-mail:bizewiseconsultancy@gmail.com

*Thanks*

Comments

Popular posts from this blog

Barua ya Kuomba Kazi

ANDIKO LA MRADI WA KUOMBA UFADHILI

Barua ya Maombi ya Kazi Kupitia Email (Barua Pepe)