ZIFAHAMU AINA ZA BIASHARA NA MIUNDO YAKE


Karibu tena mpenzi msomaji wa blog hii, nadhani mpaka sasa umeweza kupata angalau mwanga wa kujua na kuilinda biashara yako ili iwe yenye tija na yenye kukua kila siku, leo nitakwenda kuzungumzia hasa aina za biashara na muundo wake ili kukuwezesha kujua ni aina gani hasa ya biashara unafanya. Kimsingi kabisa tuna aiana kuu tatu za biashara;
  1. Biashara za huduma,(Service Business)
Hizi ni aina ya biashara ambazo hujishuguisha na mauzo ya bidhaa zisizoonekana wala kushikika mf; huduma za elim, afya, ushauri wa kitaalam, ambapo katika biashara hii pia imegawanyika katika sehem kuu tatu pia
  • Huduma za Kitaalam mf; sharia, ushauri wa maswala ya fedha n.k
  • Huduma za Kifedha(Financial Service) mf; bima, benki
  • Huduma za Mawasiliano(Information Service
  •  Biashara ya kuuza bidhaa(Merchandise Business)
Hizi ni aina za biashara ambazo hujishugulisha na kununua bidhaa kwa jumla na kuuza kwa rejareja, bidhaa hizi ni lazima ziwe zinashikika na kuonekana kwa macho, aina hii ya biashara ni maarufu kwa jina la “BIashara za kuuza na kununua”
  1. Biashara mseto(Hybrid Business)
Hizi ni aina za biashara ambazo zinakuwa zimechangamana kwa pamoja, biashara hizi huusisha pande mbili ambazo ni utoaji wa huduma na kwa muda huohuo huuza bidhaa kwahiyo mmiliki wa biashara hii inaweza kutumia huduma ambazo hazimwingizii faida ila huku akiwa anauza bidhaa ambazo zitakuwa zinamwingizia faida. Mf; unaweza ukawa unafanya biashara ya kuuza dawa za binadamu ila kwa wakati huohuo unatoa bure huduma ya ushauri wa maswala ya afya, kumbuka wapo watu ambao wao wanauza dawa tu pia wapo ambao wamejikita katika ushauri wa kitaalam juu ya afya, kwa hiyo utakuwa unapata faida katika kuuza dawa ila ile huduma ya ushauri unatoa bure.

MIUNDO YA BIASHARA
Kuna mifumo mikuu mine(4) ya kibiashara japo kuna mingine inaibuka ila inaweza kuwa inapatikana ndani ya mifumo hii tajwa;
  1. Biashara ya mtu mmoja(Sole Trade)
Hii ni biashara ambayo humilikiwa na kuendeshwa na mtu mmoja, yeye anakuwa kila kitu kwenye biashara hiyo, hasara na faida huja kwake, aina hii ya biashara humfanya mmiliki hata kuweka rehani mali zake binafsi ili kulipa madeni(Unlimited Liabilities), kama biashara ikifa au kufirisika na mmiliki akiwa na deni la nje basi mali zake binafsi huwekwa rehani ili kulipa deni mf; nyumba, shamba, vitu vya ndani n.k

  1. Biashara za ushirikiano(Partnership Business)
Hii ni biashara ambayo hujumuisha watu kuanzia 2-19 ambao watu hawa hupaswa kusaini mkataba wa ushirikiano wa kibiashara(Partnership Deed) hili ni kalabrasha ambalo huanisha utaratibu wote kuanzia mtaji wa biashara, mgawanyo na jinsi ya mjumbe kujitoa kwenye muungano husika wa biashara pia hutoa ufafanuzi juu ya aina ya washirika. Biashara za aina hii pia hukopeshwa na endapo ikifirisika basi wamiliki hupaswa kuuza mali zao binafsi binafsi ili kulipa deni(Unlimited Liabilities Partners) ila wapo pia ambao mali zao hazitaguswa kutokana na ulipaji wa deni hawa wanaitwa (Limited Liabilities Partners).
  • Kampuni(Limited or Unlimited Liabilities Company)
Biashara ya aina hii tunaigawa katika makundi mawili, makampuni binafsi ambayo kwa mujibu wa sharia ya uwanzishaji wa makampuni hapa nchini yanapswa kuundwa au kumilikiwa hisa zake na watu kuanzia 7-50 na watu hawa lazima wawe na mahusiano ya karibu sana, wawe ndugu, jamaa au marafiki na makampuni ya umma ni yale ambayo hisa zake au amana zake zinamilikiwa na watu tofauti tofauti kuanzia watu 7 mpaka kuendelea anayekuwa anamiliki idadi kubwa ya hisa ndie mwenye maamuzi makubwa Zaidi, ndani ya biashara hizi kuna vitu viwili ambavyo hutoa mwongozo wa namna yake ambavyo ni Articles Of Association na Memorandum Of Association. Kampuni ambayo huuza hisa kwa umma hutafsiriwa kama kampuni ya umma(Public Company) ambazo huuza hisa kwa watu wa karibu hutafsiriwa kama kampuni binafsi(Private Company)

  1. Biashara za ushirika(Cooperative Business)
Hizi ni biashara ambazo watu huungana kwa pamoja kwaajiri ya kufanya jambo Fulani na watu hawa huwa wana mtazamo au malengo sawa, mf; wazalishaji kadhaa ya maligafi fulani wanaweza kuungana pamoja kwa lengo la kuzalisha maligafi hizo kisha kugawana kulingana na mahitaji yao au wafanyabiashara wanaweza kuanzisha benki moja kwaajiri ya kuitumia kurahisisha maswala yao ya kifedha benki hiyo inaweza kuwa na lengo kuu la kutoa msaada wa kifedha kwa makampuni hayo au pia kusaidia mabadilishano ya biashara kama wapo ambao wanafanya biashara za kimataifa kwa hapa Tanzania kuna benki moja ya Ushirika wa Wakulima inaitwa Farmers’ Cooperative Bank, Benki hii ilianzishwa ili kusaidia wakulima kupata urahisi wa mitaji na kuuza mazao yao katika maduka ya serikali(Sociaty) za vijiji kwahiyo benki hiyo ilisimamia kila kitu cha kifedha kuhusu wakulima.
Aina zote nilizozitaja hapo juu zinafaida na hasara katika uendeshaji wake, Mungu akijaalia naweza kuzileta ili uzijue na ujue ni biashara gani inafaa wewe kuifanya au kuendelea nayo, kufikia hapa nadhani umepata mwaka kwamba ni aina gani ya biashara unafanya au unataka kuifanya.

Comments

Popular posts from this blog

Barua ya Kuomba Kazi

Jinsi ya Kuandika Ripoti

ANDIKO LA MRADI WA KUOMBA UFADHILI