ZIJUE HAPA LEO : FAIDA ZA KUFUNGUA KAMPUNI



UNATAKA KUFUNGUA KAMPUNI? HIZI NI FAIDA ZA KUFUNGUA KAMPUNI
Kama una malengo makubwa nakuomba uwaze kuwa na kampuni hata kama utashindwa kwa sasa ila baadae jitahidi.
Kufungua kampuni sio lazima uwe na mtaji, na gharama za kufungua ni ndogo sana. Angalia hapa gharama zake zilivyoanishwa na Brela. Lakini faida ya kufungua kampuni ni kubwa sana sana na ni muhimu sana.
Kwa haraka haraka, ukiwa na kampuni;
  1. Kodi inatozwa kwenye faida utakayopata (tena hata faida yenyewe unakatwa kodi yake ile faida uliyoshindwa kuitumia). Mfano. Kama niliuza mauzo ya Mil 100, na humo nilipata faida Mil 30, lakini nikanunua gari ya kampuni mil 25, basi kodi nitakatwa kwenye Mil 5.  Kwa Mtu binafsi angekatwa zaidi ya mil 10
  2. Makadirio ya kodi utafanya mwenyewe
  3. Inatambulika kisheria(legal entity).
  4. Kama una hasara hutakiwi kulipa kodi
  5. Huwezi kurisisha Kazi ya kuajiriwa, bali unaweza kurithisha Kampuni. Na pia ni rahisi kuepuka migogoro ya mirathi kama una kampuni kuliko mali binafsi
  6. Ni rahisi kukopesheka kama biashara iko vizuri au kuaminika na makampuni mengine.
  7. Ukiwa na kampuni ni rahisi kutumia mtaji wa kampuni nyingine pasipo mkopo. Yaani ni rahisi kupewa bidhaa na kampuni nyingine pasipo kulipa kwanza kwa makubariano ya kulipa baada ya kuuza (Credit facility).
Kwa hiyo ukiwa na kampuni wimbo wa sina mtaji unapotea na pia unaingia kwenye uwanja wa kula vinono. (Mfano huwezi kupata tenda ya kutengeneza barabara kama wewe sio kampuni).
KIUNDANI: FAIDA ZA KUFUNGUA KAMPUNI
  • Kuwa na kampuni kunakuwezesha kuingia katika biashara kubwa kubwa ambazo hawezi kupewa mtu binafsi (contract au tenda) na pia inafungua mlango na trust kuweza kushirikiana  na makampuni mengine, kwa kuwa makampuni yanaamini na kufanya biashara na makampuni badala ya mtu binafsi.
  • Pia ukiwa na kampuni ni rahisi kutumia mtaji wa kampuni nyingine pasipo mkopo. Yaani ni rahisi kupewa bidhaa na kampuni nyingine pasipo kulipa kwanza kwa makubariano ya kulipa baada ya kuuza (Credit facility).
Mfano kama umepewa tenda ya kusupply Mifuko 1000 ya mbolea kwenda kampuni X ya kilimo, Basi ukiwa na kampuni yako ni rahisi kampuni Y inayozalisha Mbolea hizo kukupa mzigo mbolea ukasupply kwa mteja X; na wewe ukawalipa baada ya kupewa hela. (Yaani unatumia mtaji wa manufacturer wewe kufanya biashara hata kama huna mtaji).
  • Ukiwa umesajili kampuni unakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kupata ushirikiano na hao walengwa wako kwa haraka zaidi maana wanakuwa wanaongea na kampuni na sio mtu binafsi. hii ni Kama una wazo la kutafuta wafadhili wa biashara yako.
  • Kuna makato madogo ya kodi kwasababu kampuni unakatwa kodi kiasi cha faida ulichoshindwa kutumia na sio kiasi cha mauzo yote. Yaani unakatwa kodi baada ya matumizi na sio kabla ya matumizi.
Mfano: Kama una mauzo ya Milioni 100; basi ambaye hana kampuni atakatwa zaidi ya Milioni 10 au zaidi. Lakini  kampuni unakatwa kodi kiasi cha faida tu ambacho hujatumia. Yaani kama kwenye mauzo ya Milioni 100 ulikuwa na faida ya Milioni 30;  lakini ukaitumia hiyo faida kwa matumizi ya kampuni (Mfano kununua gari ya kampuni, kuwekeza, n.k) baadaye ukabaki na Milioni 5, basi unakatwa kodi kwenye hiyo Milioni 5. Kitu ambacho hakipo kwa Mtu binafSi.
  • Chini ya kampuni moja unaweza kufanya biashara nyingi tofauti, ili linawezekana kupitia kukata leseni tofauti za biashara (business license) kulingana na shughuli unazotaka kufanya. Yaani kampuni moja inaweza kuwa na leseni za biashara zaidi ya moja.
  • Ukiwa na kampuni ni rahisi kumrithisha ndugu, mtoto au mtu wako wa karibu hizo biashara kupitia hiyo kampuni. Ukifanya biashara kama mtu binafsi inamaanisha wewe ndiyo mmiliki pekee wa hiyo biashara, yaani hautaweza kummilikisha mtu mwingine.
  • Pia unakuwa na nafasi ya kutofautisha mali zako binafsi na mali za kampuni. Hii itakusaidia pale ambapo imetokea kampuni yako inadaiwa, basi deni hilo halitafika kwenye mali zako binafsi ambazo hazimilikiwi na kampuni
SIKU UKIHITAJI KUFUNGUA; TUNATOA HUDUMA YA KUFUNGUA KAMPUNI
  1. Kuandaa MEMART. (Memorandum of Association and Articles of Association)
  2. Name search na kusajili BRELA
  3. Kukusaidia Mambo ya TRA na Manispaa
  4. MAMBO YA MPANGILIO WA MAHESABU (record keeping system) NA ACCOUNTING SOFTWARE YA KUTUNZA KUMBUKUMBU
  5. Kutengeneza Company Website or official company email (bila website). Pamoja na kufanya setup nzima ili muweze kuzitumia proffesionally bila shida.
  6. Na kuwapa mikataba ya wafanyakazi kama mtapanga kuajiri au ili kuitumia wakati wa kuajiri. (Ready made contracts)
  7. Kuwasiadia/kuwaongoza usajili wa bank account ya kampuni, NSSF, NA WCF (wokers compassion fund)
KUIJUMLA WE HELP TO REGISTER, ESTABLISH AND TO MAKE YOUR COMPANY RUN PROFESSIONALLY
Mawasiliano
0764530882 au 0626402722
ORODHA YA FURSA ULIZONAZO (kwanini usipige hatua??)
1. Kununua Mashine za kukoroga zege na
kukodisha.
2. Kununua Mashine za kukata vyuma na
kuzikodisha.
3. Kutengeneza na kuuza tofali
4. Ufundi, Website updating/Database: Katika
Halmashauri, Manispaa, Mashule, Wizara, Wilaya
na Makampuni mbalimbali.
5. ** Kuanzisha kituo cha redio na televisheni
6. Kufunga na kutengeneza vifaa mbalimbali vya
electroniki na mawasiliano mfano; compyuta na
vifaa vya compyuta na mawasiliano.
7. ** Kuuza software; mfano Antivirus, Operating
Systems, Pastel, Tally, Myob, n.k
8. Kushona na kuuza nguo.
9. Kufungua Duka la kuuza nguo mpya; suit,
socks,
batiki, nguo za asili, Mashuka, Mashati, Suruali,
10. Ufugaji wa mifugo mbalimbali mfano Kondoo,
Mbuzi, Ng?ombe, Kuku, Bata, na wengine.
11. Kufungua stationery, kuuza (supply) vitabu na
vifaa mbalimbali ktk mashule na vyuo.
12. ** Kutoa ushauri mbalimbali wa Kitaalamu.
13. Kuuza viazi, mahindi, mihogo, kutengeneza
popcorn na kuziuza.
14. Kusajili namba za simu na kuuza vocha
15. Kuwa na mradi wa Pikipiki zisizotumia mafuta
na zinazotumia mafuta
16. ** Kilimo cha mazao mbalimbali kulingana na
hali ya hewa ya sehemu husika.
17. Kuuza Mitumba
18. ** Kusimamia miradi mbalimbali
19. Kufungua duka la kuuza mitambo mbalimbali
20. Kufungua banda la chakula na chips
21. Kukodisha turubai viti na meza
22. Kufungua Supermarket
23. Kufungua Saluni
24. Kufungua Bucha
25. Video Shooting & Editing.
26. ** Kufungua Internet cafe
27. Duka la kuuza matunda
28. Kufungua duka la kuuza vifaa vya simu za
mkononi na landline.
29. Kufungua duka la vifaa vya ujenzi; cement,
vifaa
vya umeme, duka la mabati
30. Kutengeneza michoro mbalimbali ya majumba
na
miradi ya ICT
31. Kuchapa vitabu, bronchures, n.k
32. Kuanzisha kampuni ya ujenzi (Building
contractor)
33. Kuuza Vifaa vya umeme wa nishati ya jua
(solar) ,battery, inverter na vifaa vingine vya
solar n.k
34. ** Kuuza maji kwa jumla na rejaleja.
35. Kutengeneza na kuuza Unga wa lishe bora.
36. Kukodisha Music
37. Kuanzisha Mradi wa Taxi
38. ** Kuanzisha mradi wa Daladala
39. Kuuza vifaa vya Kompyuta, laptops, converters,
HDDs, Monitors, Softwares, CD Copiers na vifaa
vingine.
40. ** Kununua magenerator na kukodisha
41. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za simu
42. ** Kufungua kampuni ya kutoa huduma za
internet (ISP)
43. Kuuza mabati na vigae
44. Kujenga apartments
45. ** Kufungua Kisima cha mafuta ya taa au
mafuta ya aina zote
46. Kufungua Duka la samaki
47. Kufungua Duka la nafaka
48. ** Kufungua Shule za Awali, Shule za Msingi,
Sekondari na Vyuo.
49. Kujenga hostel
50. Kuuza vocha na ving?amuzi vya DStv, Zuku,
Startimes, Easy TV, TNG, Digitech, Continental.
51. ** Kujenga mtambo wa kuzalisha umeme na
kuuza katika viwanda na wananchi.
52. Ufundi simu
53. Kufungua Hospitali, Zahanati.
54. Maabara ya Macho, Meno
55. ** Kuchimba/Kuuza Madini
56. ** Kufungua ofisi ya kutoa huduma ya simu na
fax
57. Kuuza miti na mbao
58. Kufungua Grocery, bar
59. Kufungua studio ya kupiga na kusafisha picha
60. ** Kucharge simu/battery
61. Duka la TV na vifaa vingine
62. Kuanzisha biashara ya kuuza vyakula katika
sherehe na tamasha mbalimbali (catering).
63. ** Banda la kupigisha simu
64. Kuuza na kushona Uniform za shule
65. Kuanzisha duka la kuuza vitu kwa jumla.
66. Kufungua gereji za kutengeneza bajaji, pikipiki
na
magari
67. Kuuza vyuma, pembejeo, rake, jembe
68. Kuuza fanicha
69. Kufungua sehemu ya kuziba pancha za matairi
ya magari na mitambo.
70. Kujenga nyumba za kulala wageni (hotel)
71. Kuagiza na kuuza vifaa vya aluminium.
72. Kuuza vioo
73. Kushona na kukodisha nguo za harusi
74. ** Kufungua yard kwa ajili ya kuosha magari
75. Kuuza mashine za kuchomelea (welding
machine).
76. Kuuza vifaa vya kuvaa Site (boots, helmets etc)
77. ** Kununua mabasi kwa ajili ya kusafirisha
wanafunzi
78. Kufungua studio ya kutengeneza vipindi vya
redio na televisheni
79. ** Kuanzisha ofisi ya michezo ya televisheni
(TV
Games)
80. ** Kufungua benki
81. Kuwa na malori ya kubeba kokoto na mchanga
82. Kuuza vifaa mfano TV, CCTV Camera, n.k
83. Kuwa dalali wa vitu mbalimbali
84. Kuanzisha mradi wa kukodisha fork lift na
winchi (crane)
85. Kuanzisha kiwanda cha kutengeneza viatu.
86. ** Kuanzisha viwanda mbalimbali
87. Duka la vifaa vya simu na gadgets mbalimbali
zinazoendana na mawasiliano ya Vodacom,
TTCL, AIRTEL, TIGO, ZANTEL, n.k.
88. ** Kujenga Ukumbi wa kukodisha kwa sherehe,
mikutano mbalimbali
89. Kununua matrekta, mitambo ya ujenzi wa
barabara na kukodisha
90. Kutengeneza antenna na kuuza
91. Kufungua mradi wa Machine za kusafisha,
kutoboa na kuchana mbao
92. ** Kufungua mradi wa kuuza vifaa vya Umeme
wa kutumia upepo
93. Biashara ya kuagiza magari
94. Kufanya biashara za Jukebox
95. ** Kukodisha matenki ya maji**
96. Kufungua duka la kuuza Asali
97. Kutengeneza Mikokoteni/ matoroli na
kuikodisha
98. Kufungua Duka la vinyago, batiki
99. Kuanzisha huduma ya AIRTEL MONEY, MPESA,
TIGOPESA, EZY PESA
100. ** Kuanzisha sehemu ya kufanyia mazoezi
(Gym).
101. Kununua na kuuza vifaa vya kupima ardhi.
102. Kufungua duka la kuuza dawa (pharmacy).
103. Kufungua Kampuni ya Ulinzi
104. Kufungua kampuni ya "Clearing and
fowarding"
105. Kuchezesha vikaragosi
106. Kuuza spea za bajaji, magari na pikipiki
107. Kuuza baiskeli
108. Kuuza magodoro
109. Kuuza vyombo mbalimbali kwa ajili ya
matumizi
ya nyumbani mfano bakuli, sahani, vikombe,
vijiko,
110. Kuuza marumaru (limestones)
111. Kuuza kokoto
112. Kuuza mchanga
113. Kufundisha Tuisheni
114. Biashara za bima
115. ** Kampuni ya kusafirisha abiria kwa njia ya
anga (ndege)
116. Biashara za kitalii
117. Biashara za meli na maboti.
118. ** Kampuni ya kuchimba visima
119. Kufungua ofisi ya wakili/mawakili wa
kujitegemea
120. Kuuza mkaa
121. Kutengeneza mashine za kutengeneza tofali
122. ** Kampuni ya kupima ardhi
123. Kampuni ya magazeti
124. Kuchapa (printing) magazeti
125. Kuuza magazeti
126. ** Kuchimba mafuta
127. Kiwanda cha kutengeneza mabati
128. Kiwanda cha kutengeneza fanicha
129. Kiwanda cha kutengeneza matairi
130. Kutengeneza vitanda vya chuma
131. ** Kununua nyumba katika Maghorofa
(Apartments) na kuzikodisha.
132. Kukodisha makapeti
133. Kupamba maharusi na kumbi za harusi/
sherehe.
134. Mashine ya kusaga na kukoboa nafaka.
135. Kazi ya ususi na kusafisha kucha.
136. Kuuza Gypsum
137. Malori ya kubeba mafuta na Mizigo
138. Duka la kuuza mboga za majani
139. Duka la kuuza maua.
140. Kampuni ya kuzoa takataka
141. Kampuni ya kuuza magari
142. ** Kuuza viwanja
143. Uvuvi
144. Kutengeneza na kuuza nguzo za kujengea
fensi
145. Uchoraji wa mabango.
146. Duka la kuuza silaha
147. Ukumbi wa kuonesha mpira
148. Biashara ya mlm (network marketing)
149. ** Yadi kwa ajili ya kupaki magari
150. Mradi wa trekta za kukodisha kwa ajili ya
kilimo. 151. kutengeneza sabuni za kunawia mikono na kuziuza 152. kutengeneza dawa za kusafishia vyoo, mabafu na
kuziuza 153. kuanzisha kampuni za usafi na kutafuta tenda ktk
taasisi mbalimbal 154. kuanzisha botanical garden na kufungua duka la
chemikali na kusaka tenda mashuleni na vyuo 154. n.k,...
KAMA YOTE HAYA UMESHINDWA KUPATA LA
KUFANYA, WEWE UTAKUWA USHAPOTEA,
ENDELEA NA UTARATIBU WAKO WA KUILAUMU
SERIKALI.
Mtumie na mwenzio aone

Comments

Popular posts from this blog

Barua ya Kuomba Kazi

Jinsi ya Kuandika Ripoti

ANDIKO LA MRADI WA KUOMBA UFADHILI