ANZA HIVI 2019 -HEALTHLY, WEALTHLY AND WISE!

Rafiki yangu mpendwa,
Tayari tupo kwenye mwaka 2019, huenda uliona mwaka 2019 ni mbali sana, lakini ndiyo huo tayari umeshakuwa mwaka wetu.
Kila mwaka kwa miaka mitatu iliyopita tumekuwa na maneno matatu ya kutuongoza kwa mwaka mzima.
Haya yanakuwa ni maneno ambayo yanatuonesha kipaumbele chetu kwa mwaka husika ni kipi.
Pia ni maneno ya kujikumbusha yale maamuzi tuliyoyafanya kwa mwaka husika.
Ni maneno ambayo tunapaswa kuyatafakari na kuyaishi kila siku ili maisha yetu kuwa bora zaidi.
Maneno matatu ya kutuongoza mwaka huu 2019 yatakuwa ya tofauti kidogo.
Kwa mwaka huu 2019, maneno ya kutuongoza yatatokana na kauli ambayo pia ndiyo itakayotuongoza kwa mwaka mzima.
Kauli ambayo itatuongoza mwaka huu 2019 inatoka kwa mmoja wa waasisi wa taifa la Marekani, Benjamin Franklin ambaye aliwahi kuandika; “Early to bed and early to rise, makes a man healthy, wealthy, and wise”. Akimaanisha kuwahi kulala na kuwahi kuamka kunamfanua mtu awe na AFYA bora, UTAJIRI na HEKIMA.

Comments

Popular posts from this blog

Barua ya Kuomba Kazi

ANDIKO LA MRADI WA KUOMBA UFADHILI

Barua ya Maombi ya Kazi Kupitia Email (Barua Pepe)