Mastori ya taown

Nina rafiki yangu nimemkaribisha nyumbani kwetu tunaishi mimi na yeye tu hatujaoa nilikuwa naishi peke yangu alikuwa anaishi kwa mjomba wake nyumba ikapangishwa.

Nikaona ni vyema aje niishi nae sababu tulisaidiana mambo mengi ya kimaisha kwa miaka minne amehamia nyumbani ni miezi miwili sasa.

Wiki iliyopita alisema ameenda kwa mganga amedai analogwa sana ndo maaana mambo yake hayaendi kwa hiyo amepewa dawa na mojawapo ya dawa ni kuoga usiku wa saa 7 nje kuondoa mikosi na swala lingine na anadai kuwa huyo mganga humfuata kimiujiza akiwa amelala na kumtibu kwa njia hiyo nyumbani na mimi alinishauri kwenda kwa huyo mtalaamu nikaangalie matatizo yangu nimekataa kwenda

Sasa nataka nimwambie asiogee hizo dawa nyumbani lakini naona kama jamaa atachukia na kuona sipendi maendeleo yake hivyo nifanyeje?

Na mimi sipendi haya mambo ya kishirikina
 

Comments

Popular posts from this blog

Barua ya Kuomba Kazi

ANDIKO LA MRADI WA KUOMBA UFADHILI

Barua ya Maombi ya Kazi Kupitia Email (Barua Pepe)